Imeandikwa na: Saad Ally Nassor | Imeupdate: Julai 26, 2026
Watu wengi Tanzania wamepoteza pesa na akaunti zao mtandaoni. Wengine wameibiwa WhatsApp, wengine wamepewa link za kubonyeza na kuibiwa namba za siri OTP. Makala hii itakupa hatua 7 za kujilinda 100%.
OTP ni namba ya siri inayotumwa na M-Pesa, Bank, WhatsApp. Ukimpa mtu OTP = Umempa akaunti yako yote. Benki haiwahi kuomba OTP kwa simu.
Mfano: "Hongera umeshinda Tsh 1,000,000 bofya hapa". Hizo ni link za kuiba password yako. Angalia kama link inaandikwa `https://` na jina la kampuni.
Matapeli wanapiga wakidai ni wa Vodacom au Airtel. Wanakuomba namba ya NIDA. Kumbuka: Hakuna kampuni inayopiga kuomba taarifa zako.
Nenda WhatsApp > Settings > Account > Two-step verification. Iweke. Hata mtu akijua password yako bila hiyo code hawezi kuingia.
Kama rafiki anakuomba pesa WhatsApp, mpigie simu kwanza kuhakikisha ni yeye. Akaunti nyingi zinaibwa na kutumiwa kuomba pesa.
Kanuni ni moja: Akili yako ndio Firewall yako kubwa. Kama kitu kinakupa shaka, acha. Ni bora kupoteza fursa kuliko kupoteza pesa yako yote.